Get Paid To Promote, Get Paid To Popup, Get Paid Display Banner

KISARAWE LUTHERAN JUNIOR SEMINARY 20YEARS ANNIVERSARY

Wapendwa,

Kwa wale wote mliopita katika shule hii, kwa namna moja au nyingine hapa mahali pamechangia kwa kiasi kikubwa sana kuwa watu tulio leo. Hii shule ilianzishwa kwa nguvu za walutheran wa Tanzania, na mimi kama mmoja wa watu waliopita hapa, nakubali kabisa kwamba tuna jukumu la kupaendeleza mahali hapa, pawe mahali ambapo watoto wetu na wajukuu wetu watasoma kwa raha. Natumaini kwa nguvu zetu zote tutaweza kufanikisha kuchangia harambee ya maendeleo ya KLJS katika mwaka huu ambao shule yetu inaadhimisha miaka 20 tangu kuanzishwa kwake.

Baadhi ya wanafunzi tuliowahi kupita hapa tunapatikana kwenye page ya Facebook inaitwa KILUJUSE tafadhali ingia humu na toa mchango wako wa mawazo. Kamati ya alumni ya KILUJUSE inaandaa tarehe ya kikao cha pamoja, tafadhalini sana kwa wale wote ambao tupo hapa mjini tuguswe kufika siku hiyo. Na kwa wale walioko nje ya nchi na nje ya mkoa tutawaeleza ni jinsi gani mtaweza kuchangia katika tukio hili la kihistoria. 

Mungu awabariki sana na awaongezee maradufu pale mtakapotoa.

Karibu KILUJUSE - some of greatest people in this country originates here

early volunteers teams, our friends in Christ who helped us build our school

KILUJUSE pioneers

Nathan and other former students



some of the early students


Ngowo, Ezra, Khamsin Babu na Mr Adam, na huyo mzungu ni pastor  Wolf? not sure msaada jamani

Anna Mgelwa na classmates, enzi hizo wakiwa njuka - hii ilikua siku ya Pamba na wali bila shaka

Mwanzo mgumu jamani, KILUJUSE ilitokea hapa, hata sasa Mungu anatusaidia kwakweli

Library, KILUJUSE. Asante Mungu, Washaika wa KKT tanzania na marafiki zetu wa ELCA na Ujerumani. Mungu awabariki sana na awaongezee pale mlipotoa

Mama Margareth Bulugu na Wanafunzi wa miaka ya mwanzoni kabisa. Mungu akubariki mama na Tunakuombea Afya yako itengemae