Get Paid To Promote, Get Paid To Popup, Get Paid Display Banner

UHURU KENYATTA AJIUZULU KENYA.


Kenyan Finance Minister Uhuru Kenyatta in a file photo. President Mwai Kibaki has accepted the resignation of  Kenyatta, the presidential spokesman said on Thursday.  REUTERS/Thomas Mukoya
- Waziri wa fedha wa Kenya Bw. Uhuru Kenyatta amejiuzulu leo siku chache baada ya jina lake kuonekana katika watuhumiwa wa uchochezi wa fujo za uchaguzi wa mwaka 2007 iliyotolewa na mahakama ya kimataifaa ya makosa ya jinai (ICC) hivi karibuni.
 Kujiuzulu huko kwa Kenyatta kumeenda sambamba na kiongozi mwingine wa umma bw. Francis Muthaura.
 
 
           Hata hivyo katika kuonesha kuwa huo sio mwisho wa harakati zake katika siasa Kenyatta amehusishwa nu kugombea urais mwaka 2013 safari hii akiungana na aliyekuwa adui yake katika fujo na uchaguzi wa mwaka 2007 ndugu William Ruto ambaye pia ni mtuhumiwa wa ICC katika fujo hizo za uchaguzi wa mwaka 2007. Kenyatta na Ruto wanadaiwa kuchochea makundi ya vijana kutoka katika itikadi, makbila  na sehemu tofauti  kupigana na kuuana punde baada ya uchaguzi mkuu wa Kenya mnamo mwaka 2007 kumalizika.
 
           Kenyatta mwenye miaka 50 mtoto wa Jomo Kenyatta baba wa taifa la Kenya na tajiri zaidi Nchini Kenya alikuwa akipata shinikizo la kujiuzulu kutoka kwa wabunge wenzake kufuatia kupatikana na kesi ya kujibu na mahakama ya kimataifa ya makosa ya Jinai.
 
           Ni desturi nchini Kenya kwa mawaziri wanaotuhumiwa kwa rushwa na matumizi mabaya ya ofisi za umma kujiuzulu ingawa Mwanasheria mkuu wa Kenya Kenyatta and Muthaura wangeweza kuendelea na nafasi zao mpaka hapo rufaa walizokata kwa mahakama hiyo ya kimataifa kukataliwa suala ambalo huchukua hadi mwaka mmoja.